.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 13 Agosti 2015

MJUMBE WA UN KATIKA NCHI YA JAMHURI YA AFRIKA YA KATI (CAR) AMEFUKUZWA KAZI

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika nchi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) Babacar Gaye amefukuzwa kazi kufuatia matukio maradufu ya udhalilishaji wa kingono yaliyofanywa na walinda amani.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amewaambia waandishi wa habari umoja huo umeomba barua yake ya kujiuzulu.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja tu kupita tangu shirika la Amnesty International kudai kuwa mtoto wa kike wa miaka 12 alibakwa na wanajeshi wa Umoja wa Mataifa.

Kikosi cha wanajeshi 10,000 cha Umoja wa Mataifa kiliwekwa CAR mwaka jana kujaribu kurejesha utulivu, lakini sasa kinakabiliwa na tuhuma za kufanya ukatili wa kingono kwa watoto wa mitaani.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni