.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 24 Mei 2016

MGOMO WA KUPINGA SHERIA ZA KAZI WASABABISHA UHABA WA MAFUTA UFARANSA

Mgomo wa kupinga sheria mpya za kazi nchini Ufaransa umesambaa katika mitambo yote minane ya kusafishia mafuta ghafi umoja wa wafanyakazi umesema na kukuza mgogoro na serikali.

Kutokana na kufungwa kwa njia za kwenda kwa mitambo ya kusafishia mafuta ghafi asilimia 20 ya vituo vya mafuta nchini Ufaransa vimeishiwa na mafuta kutokana na kukosa mafuta yanayoingizwa.

Waziri Mkuu wa Ufaransa, Manuel Valls, amesisitiza sheria za kazi mpya hazitaondolewa, na vikosi vya usalama vitayasambaratisha makundi yanayozuia njia za mitambo ya kusafishia mafuta.
   Polisi wakihangaika kuondoa kizuizi katika moja ya barabara ya mtambo wa kusafishia mafuta ghafi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni