.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 29 Januari 2017

WACHIMBAJI MADINI 15 WALIOFUKIWA NA KIFUSI WAOKOLEWA WAKIWA HAI

Wachimbaji 15 waliokuwa wamefukiwa na kifusi katika mgodi wa dhahabu wa RZ uliopo Nyarugusu, Mkoani Geita nchini Tanzania wameokolewa wote leo asubuhi wakiwa hai.

Wachimbaji hao walifukiwa na kifusi tangu siku ya Alhamis wamefanikiwa kuokolewa kufutia jitihada zilizofanywa na waokoaji bila kukata tamaa na hatimae kuzaa matunda leo.

Hapo jana vikosi vya uokoaji vilifanikiwa kushusha chini aridhini tochi na radio kwa kutumia drill na kamba ikarudi tupu wakajua vitu hivyo vimepokelewa.

Wakashusha barua, kalamu na karatasi na vipapokelewa na kujibiwa kwa maandishi kuwa wachimbaji hao wapo 15 na mmoja wao ameumia kwa kuchomwa na msumari.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni