.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 23 Machi 2017

SERIKALI ITOE KWA WAKATI FEDHA ZA MRADI WA UJENZI JENGO LA TATU LA ABIRIA UWANJA WA NDEGE WA MWAILIMU NYERERE, KAMATI YASISITIZA


KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeitaka serikali kuhakikisha inatoa kwa wakati fedha za mradi wa ujenzi wa Mradi wa jengo la tatu la abiria (TB III) la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, ili mradi huo uweze kukamilika Disemba 2017 kama ilivyopangwa.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Norman Sigalla alitoa kauli hiyo leo wakati wa kufanya majumuisho baada ya kutembelea na kuona maendeleo ya ujenzi huo, ambapo ukikamilika jengo hilo litakuwa na uwezo wa kupokeo abiria milioni 6 kwa mwaka.

Prof. Sigalla alisema kukamilika kwa jengo hilo kwa wakati utapunguza msongamano wa abiria ambao sasa wanahudumiwa kwenye jengo la pili la abiria la JNIA (TBII).

uliopangwa utawapa heshima Watanzania lakini pia kupunguza msongamano katika jengo la sasa la Terminal II.

“Ninawapongeza sana ten asana kwa ujenzi wa jengo hili ikimalizika ninaimani kubwa litatupa heshima kubwa, hivyo ili likamilike kwa haraka tunaiomba serikali yetu itoe fedha kwa wakati kwani tumeona ndio moja ya changamoto zilizozungumziwa hapa,” alisema Prof. Sigalla.

Aliongeza kuwa … “pato la taifa litaongezeka kwa ndege nyingi za nje na kubwa zitakapokuja kutua kwenye kiwanja chetu,”.

Awali wakati akisoma taarifa fupi ya ujenzi wa jengo hilo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Salim Msangi alisema, changamoto kubwa inayowakumba ni serikali kuchekewa kutoa fedha.

Bw. Msangi alisema changamoto nyingine ni sheria ya Mamlaka ya Mapato (TRA) ya kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ilipitishwa mwaka 2015, awali kabla ya sheria hiyo kupitishwa vifaa vya ujenzi wa jingo hilo vilikuwa na msamaha wa kodi, lakini baada ya kupitishwa msamaha huo uliondolewa na kusababisha baadhi ya vifaa kukaa kwa muda mrefu bandarini baada ya kuzuiwa.

Alisema kutokana na changamoto hiyo ya kuchelewa kwa fedha na vifaa kukwama bandarini, kumesababisha mradi huo uliokuwa umepangwa awali kumalizika Agosti 2016 kushindwa kukamilika kwa wakati na sasa unatarajiwa kukamilika Disemba 2017.

“Tunaiomba serikali itusaidie upatikanaji wa fedha hizi za mradi kwani hii ni moja ya changamoto kubwa inayotishia kuendelea kwa ujenzi huu,” alisema Bw. Msangi.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi), Dk Leonard Chamriho alieleza juu ya notisi iliyotolewa na Mhandisi Mshauri ya kutaka kusitisha huduma kuanzia leo (Jumatano) hadi atakapiliwa fedha anazodai.

“Tayari serikali imeanza kufanyia kazi deni hili na sasa ipo kwenye hatua nzuri ya kuhakiki nyaraka za malipo kabla ya kumlipa,” alisema.

IMETOLEWA NA BAHATI MOLLEL, AFISA UHUSIANO MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA (TAA0.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni