.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 3 Aprili 2017

ARSENAL YALAZIMISHA SARE DHIDI YA MANCHESTER CITY IKIWA NYUMBANI

Timu ya Arsenal imelazimika kutokea nyuma mara mbili na kulazimisha sare ya magoli 2-2 dhidi ya Manchester City katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza kwenye dimba la Emirates.

Katika mchezo huo wageni City waliandika goli la kwanza katika dakika ya tano tu kupitia kwa Mjerumani Leroy Sane akipiga mpira baada ya kumzunguka kipa David Ospina.

Hata hivyo Theo Walcott aliisawazishia Arsenal dakika tano kabla ya mapumziko baada ya kuua mtego wa kuotea.

Manchester City waliongeza goli la pili kupitia kwa Sergio Aguero lakini goli hilo pia lilisawazishwa kupitia kwa Shkodran Mustafi kwa mpira wa kichwa.
                                     Leroy Sane akiwa amenzunguka kioa Ospina na kufunga goli 
                               Shkodran Mustafi akifunga goli la pili na kuisawazishia Arsenal

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni