.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 20 Aprili 2017

BARCELONA YASHINDWA KUFANYA MIUJIZA YATOLEWA NA JUVENTUS UEFA

Timu ya Juventus imeweza kucheza mpira safi wa kujihami na kufanikiwa kutinga nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuilazimisha sare tasa Barcelona katika dimba la Nou Camp.

Ikiwa ishafungwa 3-0 katika mchezo wa awali, Barcelona ilishindwa kufanya miujiza iliyoifanya katika hatua ya 16 bora baada ya kuitoa Paris St-Germain licha ya kufunga 4-0 katika mchezo wa awali.

Lionel Messi, ambaye awali awali alinyimwa goli na kipa Gianluigi Buffon, alipiga mashuti kadhaa yaliyopotea kwa kutoka njea huku Luis Suarez na Neymar walipoteza nafasi za kufunga usiku wa jana.
                                     Lionel Messi akiangukia uso baada ya kukabiliana na Pjanic 
             Neymar akibembelezwa na mchezaji mwenzake wa zamani wa Barcelona Dani Alves 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni