Celta Vigo imetinga nusu fainali ya
Ligi ya Uropa na kuitoa timu ya Mbwana Samatta ya Genk kwa ushindi wa
magoli ya jumla 4-1, baada ya jana kutoka sare ya 1-1.
Celta Vigo ilikuwa ishapata ushindi
wa magoli 3-2 katika mchezo wa awali dhidi ya Genk na kujiweka katika
nafasi nzuri ya kusonga mbele.
Katika mchezo wa jana Pione Sisto
alikuwa wa kwanza kuifungia goli Celta Vigo katika dakika ya 63
lakini Leandro Trossard alisawazisha dakika nne baadaye.
Pione Sisto akiachia shuti na kuifungia Celta Vigo goli katika mchezo huo
Leandro Trossard akishangilia baada ya kuifungia Genk goli la kusawazisha huku Mbwana Samatta akiangalia
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni