.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 13 Agosti 2013

BIBI HARUSI MTARAJIWA AUWAWA AKINUNUA PETE YA NDOA JIJINI NAIROBI


                                     Polisi wakiutoa dukani mwili wa Beatrice Adhiambo

Watu wenye silaha wamemuua bibi harusi mtarajiwa kwa kumpiga risasi jana akiwa kwenye duka aliloenda kununua pete ya harusi kwenye jengo la Corner katika wilaya ya Kati ya Biashara Jijini Nairobi, nchini Kenya.

Bibi harusi huyo mtarajiwa Beatrice Adhiambo Nyaoke, ambaye ni mama wa watoto wanne aliuwawa ndani ya duka baada ya kupigwa risasi ambapo shemeji yake wa kiume alijeruhiwa kichwani.

Mumewe Newton Nyaoke alifanikiwa kunusurika bila jeraha lolote katika tukio hilo lililotokea jana majira ya saa kumi jioni, na kubadilisha mipango ya harusi kugeuka kuwa msiba.

Newton na marehemu Beatrice walipanga kufunga ndoa siku ya jumamosi kwenye kanisa la Mtakatifu Christopher lililopo Mathare Kaskazini.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni