Mtoto Messiah DeShwan Martin
Jaji mmoja huko Tennessee nchini
Marekani amewaagiza wazazi wa mtoto wa kiume mwenye umri wa miezi
saba kubadili jina lake la Messiah na kuwa Martin, kufuatia mgogoro
wa kiimani uliotokana na jina la Messiah.
Katika uamuzi wake huo Jaji Lu Ann
Ballew ameeleza kuwa ni mtu mmoja tu anayestahiki kuitwa Messiah naye
ni Yesu Kristo.
Hata hivyo uamuzi huo wa Jaji Ballew
umeonekana kutomfurahisha mama mzazi Jaleesa Martin ambaye anasisitiza mtoto wake aitwe
Messiah DeShwan Martin, na ameahidi kukata rufaa kwenye mahakama ya
ngazi ya juu.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni