Oprah Winfrey
Mtangazaji mahiri wa vipindi vya
televisheni, Oprah Winfrey amesema alijikuta akikumbana na kitendo
cha kibaguzi alipokuwa kwenye ziara yake hivi karibuni nchini
Switzerland.
Winfrey amesema mmoja wa wahudumu
katika duka moja kubwa la bidhaa Jijini Zurich alikataa kumuhudumia.
Winfrey, ambaye ni miongoni mwa
wanawake matajiri duniani, aliambiwa na muhudumu huyo kuwa begi
alilokuwa anataka kununua lilikuwa ni la bei ghali mno ambayo yeye
hawezi kumudu kununua.
Madai hayo ya Winfrey ameyatoa kwenye
kipindi cha televisheni, huku kukiwa na mvutano wa kisiasa katika
baadhi ya miji ya Swiss juu ya kuwazuia wahamiaji kuingia kwenye
baadhi ya maeneo ya huduma za umma.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni