Watalii wawili wanawake raia wa
Uingereza waliokuwa kwenye matembezi yao jana jioni eneo la Mji
Mkongwe visiwani Zanzibar wamejeruhiwa vibaya baada ya kumwagiwa
tindikali na watu wasiojulikana waliokuwa na usafiri wa pikipiki aina
ya Vespa.
Taarifa zaidi kutoka visiwani humo
zinasema watalii hao walikuwa katika matembezi yao ya kawaida
kujionea mji huo, ndipo ghafla wakatokea watu hao na kuwamwagia
tindikali usoni na kisha kukimbia.
Watalii hao wamesafirishwa kuja Dar es
Salaam kwa matibabu zaidi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni