
Kilimanjaro Stars ya Tanzania Bara imemaliza michuano ya kuwania kombe la Cecafa inayofanyika huko nchini Kenya kwa kushika nafasi ya nne huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na wageni katika michuano hiyo Chipolopolo ya Zambia.
Zambia ilibidi kusubiri hadi hatua ya kupigiana mikwaju ya penati ili kushika nafasi hiyo ya tatu baada ya kumaliza dakika 90 za mchezo ikiwa imefungana na Kilimajaro Stars 1 - 1.
Zambia ilipata penati 6 dhidi ya 5 za Kilimanjaro. Katika hatua hiyo ya kupigiana penati, Zambia ilikosa penati mbili huku Kilimanjaro Stars ikikosa penati tatu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni