.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 13 Desemba 2013

MASTAA WA SIKINDE KUSHUKA NA NYIMBO 5 TAMASHA LA GURUMO TCC CLUB KESHO JUMAMOSI

                  Abdallah Gama na Shakashia wakijifua tayari kwa onyesho hilo kesho
                            Maalim Gurumo ( katikati ) akifuatilia mazoezi hayo
                     Hafsa Kazinja, Edo Sanga, Juma Katundu na Jumbe wakijifua
Jumbe na Juma Katundu wakiteta jambo kuelekea tamasha la Gurumo kesho TCC Club
                     King Maluu na Yahaya wakipuliza mdomo wa bata " saxaphone "
 Komandoo Hamza Kalala naye atakuwepo hiyo kesho TCC Club Chang'ombe
                 Mpiga drum Mashaka akifanya vitu vyake katika mazoezi hayo

Mazoezi hayo makali yalifanyika Amana Club ambako kwa wiki nzima wanamuziki watakaoshiriki tamasha hilo wamekuwa wakikutana hapo na kupiga mazoezi ya kufa mtu.

Baadhi ya nyimbo hizo ni pamoja na “Selina” utunzi wake Gurumo kwa kushirikiana na marehemu Joseph Mulenga, “Barua kutoka kwa Mama” uliotungwa na Cosmas Chidumule na “Gama” (Tshimanga Kalala Assossa).
Mratibu wa mazoezi hayo, Mzee Kassim Mapili alisema nyimbo mbili zingine za Sikinde zitajulikana siku ya onyesho lakini akafichua kuwa zitakuwa ni kati ya “Neema” (Chidumule), “Supu umeitia nazi” (Karama Legesu), “Nachechemea” na “Isaya” (Hussein Jumbe).
Wasanii waliowahi kuitumikia Sikinde ambao watakuwepo kumsindikiza Gurumo ni pamoja na Cosmas Chidumule, Abdallah Gama, Hussein Jumbe, Mashaka Shaaban, Kalamazoo, Henry Mkanyia na Karama Legesu. Wengine ni Ali Yahaya na Boniface Kachala, Tshimanga Kalala Assossa, Shaaban Lendi na Ibrahim Mwinchande.
Katika maendeleo mengine, Komandoo Hamza Kalala naye kwa kushirikiana na wakongwe hao, amekamilisha mazoezi ya nyimbo mbili “Vicky” na “Tumezaliwa wote Kijiji kimoja” ambazo zitapigwa Jumamosi kusindikiza tamasha hilo.
Mkongwe Mzee Makassy nae katika tamasha hilo atashuka na wimbo wake uliowahi kutamba sana “Anifa”.
Tamasha la Gurumo 53 ni maalum kwa ajili ya kuhitimisha miaka 53 ya utumishi uliotukuka katika muziki wa dansi kwa Muhidin Maalim Gurumo ambaye ametangaza rasmi kustaafu muziki.
Wasanii wengine wanaoshiriki mazoezi hayo ni Miraji Shakashia, Hafsa Kazinja, Juma Katundu, Edo Sanga Majengo na King Maluu.
Burudani zingine zitakazokuwepo siku hiyo ni pamoja na bendi za Msondo Ngoma Music Band, Talent Band, na Twanga Pepeta.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni