.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 12 Desemba 2013

NSSF YAPONGEZWA KWA USHIRIKIANO NA WAJASIRIAMALI

 
 NSSF Tanzania imekuwa mstari wa mbele kushirikiana na wajasiriamali ili kuongeza zaidi elimu kwa wajasiriamali kuhusu Mfuko huo wa Hifadhi ya Jamii pamoja na mafao yake yakiwemo ya matibabu, uzazi, kuumia kazini na Mikopo ya SACCOS. Balozi alitoa pongezi kwa Shirika hili pamoja na Taasisi za MKURABITA, TFDA, TanTRADE zinazoshiriki kutoka Tanzania chini ya Wizara ya Afrika Mashariki na Wizara ya Kazi.
 
 Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limeonyesha tena njia kwa wadau wa sekta kwa kuvuka tena mipaka na kueneza elimu kwa wajasiriamali wa Tanzania na Afrika Mashariki washiriki wa maonesho maarufu yajulikanayo kama Jua Kali/ Nguvu Kazi Exhibition ambayo hufanywa mara moja kwa mwaka katika nchi za umoja wa Afrika ya Mashariki.

NSSF imeshiriki kwa mara ya nne katika maonesho haya kwa nia mya kuongeza wigo wa wanachama katika mfuko huo. Shirika hili linatoa mafao saba kwa mujibu wa tamko la Kimataifa la Shirikisho la Kazi Duniani (ILO). Mafao haya yakiwemo ya matibabu bure kwa Mwanachama na wategemezi wake, mafao ya Kuumia kazini,  mafao ya uzazi, na Mikopo kwa wanachama hutolewa wakati wakiwa kazini na mafao ya muda mrefu kwa mtindo wa pensheni hutolewa pindi vigezo vikikamilika. Pensheni husika ni ya Uzeeni, ya Ulemavu na ya Urithi.

Mafao haya ya Muda mfupi hayapunguzi kiwango cha Pensheni itakayotolewa itakapojiri.  Meneja Kiongozi Uhusiano, Bi Eunice Chiume alinukuliwa akieleza haya katika maonesho haya muhimu ya wajasiriamali.

NSSF inawatangazia FURSA mbalimbali wadau wote wa sekta binafsi wakiwemo Wajasiriamali na Wakulima zinazopatikana kwa kujiunga na uanachama wa Shirika hili.
 
NSSF pia imetoa FURSA kwa  Watanzania wote waishio ughaibuni kujiunga na Mifuko huu kwa mfumo wa WESTADI na kuwawezesha kupata mafao ya matibabu kwa Wategemezi wanne waliopo Tanzania na usafirshaji wa mwili mwanachama anapofariki nje ya nchi.




Hakuna maoni :

Chapisha Maoni