Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Kongo (DRC) na waasi wa M23 jana wametia saini azimio linaloelezea
hatua za kumaliza mapigano katika nchi hiyo.
Nakala ya mwisho ya makubaliano hayo
iliyotiwa saini na Rais Yoweri Museveni na Rais Joyce Banda wa Malawi
Jijini Nairobi, inaelezea hatua za kumaliza mapigano zilizokubaliwa
kwenye mazungumzo yaliyofanyika Jijini Kampala.
Marais hao wamesaini nakala za
makubaliano hayo katika Ikulu ya Nairobi, akiwemo rais Joseph Kabila
wa DRC, ambao walikuwa nchini Kenya kuhudhuria sherehe za maadhimisho
ya miaka 50 ya Uhuru wa Kenya.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni