Askari wa kulinda
amani wa Umoja wa Mataifa wamesema zaidi ya watu 20, wakiwemo
wanawake na watoto wameuwawa Mashariki wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Congo.
Wengi wao
wameuwawa kwa kukatwa kwa mapanga siku ya Ijumaa na Jumamosi katika
vijiji viwili Kaskazini mwa Kivu, ikiwemo wasichana wawili waliobakwa
na kisha kukatwa vichwa.
Haijulikani ni
nani hasa aliyeendesha shambulio hilo, lakini Umoja wa Mataifa
umesema lazima wauaji hao waadhibiwe.
Kuna karibu
vikundi 10 vya waasi katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
vinavyoendesha shughuli za uasi nchini humo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni