Meneja Uhusiano wa Multchoice, Barbara Kambogi akiongea na waandishi wa habari pamoja na wadau mbalimbali wakati wa hafla hiyo.
Kushoto mwandishi wa habari wa Radio Times Adamu Husen.akiwa pamoja na wadau wengine kwenye hafla hiyo
Mmoja wa washindi
wa shindano la kuwasaka wanafunzi wakali wa uandishi wa insha na
uchoraji nchini linaloendeshwa na Kampuni ya MultiChoice kila mwaka akipewa zawadi
Baadhi ya wanahabari wakiwa katika hafla hiyo.
Fransisco
Kibasa na Maghma Jammadas wameibuka washindi wa shindano la kuwasaka
wanafunzi wakali wa uandishi wa insha na uchoraji nchini linaloendeshwa na
Kampuni ya MultiChoice kila mwaka.
Meneja Uhusiano na kampuni hiyo, Barbara Kambogi aliwatangaza rasmi
washindi katika hafla maalum ya wanahabari iliyofanyika jijini Dar es
Salaam Disemba 12-2013.
“Kwa
kutambua umuhimu wa elimu, MultiChoice imeamua kuwa bega kwa bega na
Serikali kuhakikisha Watanzania wengi wananufaika na mfumo mpya wa elimu
ambao ni wa kisayansi zaidi. Shule wanazotoka wanafunzi hawa
tumezipatia pia zawadi maalum ya dishi na kisimbuzi ambacho kina channel
maalum nane za elimu,” alisema Barbara.
Kibasa, mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mzunzumbe, Morogoro, aliibuka
mshindi wa insha nzuri ya masuala ya satelaiti akifuatwa na Fabian Shayo
kutoka shule hiyo pia. Kwa ushindi huo, Kibasa na wazazi wake watapata
ofa ya kwenda Afrika Kusini mwakani kuangalia namna matangazo ya
satelaiti yanavyorushwa.
Kwa upande wake, Maghma aliyeshinda uchoraji wa picha nzuri za satelaiti
akifuatwa na Sanjma Joshi (wote kutoka Shule ya Sekondari Agha Khan
Mzizima, Dar es Salaam), atasafiri na wazazi wake kwenda nchibni
Ufaransa kuangalia namna roketi inavyorushwa angani.
Hafla hiyo iliyohudhuriwa na waharirir ma waandishi wa habari za michezo
na burudani nchini, ilinogeshwa na wachezadansi wa Kundi la THT.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni