.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 30 Januari 2014

MAREKANI YAONYA TISHIO LA SHAMBULIO LA UGAIDI KENYA

Majasusi wa Marekani wameonya kuwa kundi la wapiganaji wa Somalia la al-Shabaab huenda linapanga jaribio la kuishambulia Kenya.

Ulinzi umeimarishwa na jitihada za kukabiliana na ugaidi nchini Kenya zimeongezwa pamoja na nchi nyingine za Afrika Mashariki tangu tukio la mauaji kwenye jengo la Westgate Jijini Nairobi Septemba mwaka jana.

Hata hivyo Kamati ya Intelijensia ya Marekani imesema nchi za Afrika Mashariki zitapata muda mgumu kukabiliana na matukio mbalimbali ya majaribio ya kushambuliwa na magaidi.

Kundi la al-Shabaab pia limeelezwa kuwa linapanga mashambulio kwenye nchi za Burundi, Djibouti, Ethiopia pamoja na Uganda kutokana na nchi hizo kuwa na wanajeshi wake katika kikosi cha Umoja wa Afrika kilichopo Somalia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni