.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 28 Januari 2014

MWANAHARAKATI WA UBAGUZI WA RANGI BI.MAMPHELA RAMPHELE KUWANIA URAIS AFRIKA KUSINI

                           Mamphela Ramphele (kushoto) akiwa na Helen Zille

Chama kikuu cha upinzani nchini Afrika Kusini,(Democratic Alliance) kimemtangaza Dr Mamphela Ramphele ambaye pia alikuwa mwanaharakati dhidi ya ubaguzi wa rangi kuwa mgombea wake wa uchaguzi mkuu mwezi Aprili.

Bi Ramphele, aliyekuwa mwandanani wa mpigania uhuru Steve Biko, aliunda chama chake cha kisiasa cha Agang mwaka jana.

Kiongozi wa chama cha Democratic Alliance, Helen Zille alisema hakuna mwanasiasa mwingine mwenye uwezo wa kutawala nchi hiyo kama Bi Ramphele.

Wadadisi wanasema kuwa hatua hii inalenga kuondoa tuhuma kuwa chama cha DA kina ufuasi mkubwa wa waafrika wazungu na kwamba hakiwezi kupata ushindi kwa hilo.

Viongozi hao wawili walisema kuwa kuungana kwao kutaleta umoja miongoni mwa wananchi Afrika Kusini , umoja ambao marehemu Mandela alipigania.

Bi Ramphele, mwenye umri wa miaka 66, anaonekana kama mtu mwenye ajenda nzuri na pia anasifika kwa vita dhidi ya ubaguzi wa rangi baadhi ya mambo ambayo yanawashawishi watu kupiga kura.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni