.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 30 Januari 2014

MWANAMUZIKI JUSTIN BIEBER AZIDI KUJITIA MATATANI NA VYOMBO VYA DOLA

                             Bieber akishuka kwenye gari kuelekea Mahakamani

Mwanamziki Justin Bieber ameendela kuandamwa na matukio, ambapo safari hii amefunguliwa mashtaka ya kumpiga dereva wa gari la kifahari la kukodisha maarufu kama limouseine, tukio ambalo ameripotiwa kulifanya mwezi DEsemba mwaka uliopita nchini Canada.

Bieber mwenye umri wa miaka 19 tu, amesababisha umati mkubwa wa mashabiki pamoja na waandishi katika kituo cha polisi huko Jijini Toronto kuripoti kwa ajili ya shitaka lake hili ambalo mwanasheria wake amesema kuwa hana hatia.

Kwa mujibu wa shtaka hili jipya, Bieber pamoja na mwenzake wameripotiwa kuhusika katika kumtolea maneno makali pamoja na kumpiga kisogoni dereva huyo siku ya tukio, na kesi hii itaanza kusikilizwa mahakamani tarehe 10 mwezi Machi.

Wakati hayo yakijiri Rais Barack Obama wa Marekani anakabiliwa na shinikizo la kumtaka kufikiria uwezekano wa kumtimua Marekani Bieber kutokana na tabia yake mbaya ya kuvunja sheria.



Hakuna maoni :

Chapisha Maoni