Askari wapya
waliomaliza mafunzo ya miezi mine katika Hifadhi ya Taifa Katavi wakipiga
saluti kabla ya kuwasilisha risala yao kwa Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan
Kijazi aliyekuwa mgeni rasmi
Mmoja wa
wakufunzi wa mafunzo Sajini Taji Simon Mbunda akipokea zawadi yake
iliyotolewa na wahitimu kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi.
Mmoja wa
wakufunzi wa mafunzo Sajini Taji Simon Mbunda akipokea zawadi yake
iliyotolewa na wahitimu kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Allan Kijazi.
Sehemu ya askari
waliohitimu mafunzo ya miezi minne kwa askari waajiriwa wapya
wakimsikiliza mgeni rasmi.
Mkurugenzi wa
Utumishi na Utawala wa TANAPA Bi. Witness Shoo akitoa nasaha zake kwa
wahitimu wa mafunzo hayo.
Mkurugenzi wa
Uhifadhi na Ikolojia wa TANAPA Bw. Martin Loibooki akiongea machache kabla
ya kumkaribisha mgeni rasmi kufunga mafunzo hayo.
Mkurugenzi
Mkuu wa TANAPA aliyasema hayo mwishoni mwa wiki alipokuwa akifunga rasmi
mafunzo ya askari wapya 96 walioajiriwa na TANAPA na kuhudhuria mafunzo ya miezi
minne katika Hifadhi ya Taifa Katavi mwishoni mwa wiki.
Kijazi
alisema kuwa TANAPA imeanzisha utaratibu mpya ambapo sasa askari wanaoajiriwa
na shirika kutoka katika Vyuo vya Wanyamapori vya Mweka na Pasiansi pamoja na
wale wa kutoka Jeshi la Kujenga Taifa watalazimika kupitia mafunzo maalum
yanayoandaliwa na shirika kwa ajili ya kuwawezesha waajiriwa wapya kufahamu
mazingira halisi ya utendaji kazi katika eneo la uhifadhi katika maeneo ya
Hifadhi za Taifa.
Wahitimu wakionyesha igizo la namna ujangili unavyoendelea na mbinu za askari katika kukabiliana na vitendo hivyo vya ujangili katika maeneo ya hifadhi.






Hakuna maoni :
Chapisha Maoni