Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ikishirikiana na wadau
wake kuanzia kesho wanatarajia kuanza kutoa huduma kwa saa 24, siku saba za
wiki, mwaka mzima bila kupumzika.
Ofisa Uhusiano wa TPA, Janeth Zurangi amesema uamuzi huo
ambao unakusudia kuongeza ufanisi wa bandari hiyo, umefikiwa baada ya wadau
mbalimbali kutia saini mikataba ya utekelezaji kazi hiyo.
Zurangi amesema ingawa kulikuwapo mabishano kuhusu vipengele
kadhaa ndani ya mkataba huo, wadau wote walikubali kuanza kutoa huduma kila
siku kwa saa 24 kuanzia Machi Mosi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni