.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 11 Aprili 2014

ABIRIA WA KQ WANUSURIKA,NDEGE YATUA NJE YA MSTARI UWANJA WA NDEGE WA JK NYERERE DAR

Abiria wakishuka kwa dharura ( kutumia ngazi kama inavyonekana ) kutoka katika ndege ya Shirika la Ndege la Kenya ( KQ ) katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere leo mchana baada ya ndege hiyo kutua nje ya njia rasmi ya kutua na kurukia ndege. 

Sababu ya ndege hiyo kutua nje ya njia yake ni kutokana na mvua kubwa zilizoendelea kunyesha katika jiji la Dar es Salaam hivyo rubani kushindwa kuona vizuri. 

Hali hiyo ilisababisha ndege nyingine zilizokuwa zinapaswa kutua au kupaa kuzuiwa kwa muda. Taarifa toka uwanjani hapo zinasema hakuna madhara yeyote kwa binaadamu, zaidi ya injini ya kulia ya ndege hiyo kupata hitilafu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni