Abiria sita wakiwemo watoto wawili
wamekufa wakati basi la abiria maarufu kwa jina la matatu nchini Kenya, lilipogongana
na lori katika eneo la Kinungi barabara kuu ya Naivasha-Nairobi.
Abiria wengine kadhaa waliokuwemo
kwenye basi hilo wamepata majeraha na wamekimbizwa katika hospitali ya Misheni
ya Kijabe kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Abiria hao sita walikufa papo hapo
katika ajali hiyo iliyotokea leo majira ya saa 12:30 alfajiri.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni