.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 13 Aprili 2014

BONDIA MANNY PACQUIAO AMDUNDA TIMOTHY BRADLEY KWA POINTI

Bondia Manny Pacquiao amemdunda Timothy Bradley kwa pointi na kushinda mkanda wa WBO wa uzito wa welterweight Jijini Las Vegas, Nchini Marekani.

Mfilipino Pacquiao ambaye alipoteza mchezo wake dhidi ya Mmarekani Bradley katika pambano lililogubikwa na utata mwaka 2012 , safari hii alitangazwa mshindi na majaji wote watatu.

Akiongelea ushindi huo wa usiku wa jana Pacquiao amesema amethibitisha kuwa safari yake ya ubondia itaendelea kuwa njema, huku Bradley akisema amejaribu lakini ndio hivyo amepoteza mchezo huo dhidi bondia bora duniani.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni