Kapteni wa feri ya Korea Kusini iliyozama amesema alichelewa kutoa amri ya kuondolewa abiria katika kivuko hicho kutokana na kuhofia abiria kusombwa na maji.
Kapteni huyo Lee Joon-seok, 69, alikamatwa siku ya Ijumaa yeye pamoja na wenzake wawili waliokuwa wakiongoza chombo hicho.
Wazamiaji wameona miili mitatu kwenye feri hiyo lakini wameshindwa kuikwamua. Idadi ya watu waliopotea ni 273 huku 29 wakithibitishwa kufa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni