Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana
akiangalia mto Malagalasi ambao ni mpaka kati ya Tanzania na Burundi
alipokuwa katika ziara wilayani Buhigwe mkoani Kigoma leo Alhamisi,
Aprili 10, 2014. Kinana yupo katika ziara ya siku tano mkoani humo ya
kukagua uhai wa Chama na kusikiliza kero za wananchi mkoani humo.
Moja ya kero kwenye mpaka huo unaokutanisha vijiji vya Kibande
(Tanzania) na Murambi (Burundi) ni Watanzania kulazimika kukumbana na
adha ya kuvuka mto huo kwenda kufanya biashara na kununua mahitaji
kwenye soko lililopo upande wa Burundi. Wapili kushoto ni Katibu wa
NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Kinana akitazama mpaka huo na namna
wananchi walivyokuwa wakivuka na wengine kushwa kwenye mto wa
Malagarasi wakitoka Burundi kuingia Tanzania.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape
Nnauye akiwa pembezoni mwa mto Malagarasi, mpakani mwa Tanzania na
Burundi wakati wa ziara hiyo.






Hakuna maoni :
Chapisha Maoni