Mwendesha mashtaka Gerrie Nel
ameendelea kumshutumu Oscar Pistorius, kwa kumtuhumu kwa kudanganya
na kutengeneza ushahidi, katika kesi ya mauaji inayoendelea katika
Mahakama Kuu ya Gauteng Mji wa Pretoria leo asubuhi.
Nel amedai kuwa Pistorius aliizima
alamu yake baada ya kuondoka chumbani na kushuku ngazi kuelekea eneo
la chini ya nyumba yake baada ya kumpiga risasi mpenzi wake Reeva
Steenkamp katika nyumba yake hiyo iliyopo mji wa Pretoria siku ya
Februari 14 mwaka jana.
Baada ya kubanwa na mwendesha mashtaka
Pistorius alikiri alifanya makosa katika maelezo yake kuhusu kuzima
alamu.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni