Timu ya soka ya Liverpool leo imeendelea kufufua matumaini ya kuutwaa ubingwa wa ligi kuu nchini Uingereza baada ya ya kuifunga Manchester City mabao 3-2 katika mchezo uliokuwa mkali huku Liverpool wakionekana kuukamia zaidi.
Mabao ya Sterling kunako dakika ya 6, Skrltel dakika ya 26 na Coutinho 78 yalitosha kuwafanya Liverpool kufikisha pointi 77 katika msimamo wa ligi kuu Uingereza na kuongoza ligi hiyo.
Manchester City ambao walipambana na kupata mabo mawili yaliyowekwa kimiani na Silva dakika ya 57 na bao la kujifunga la beki wa Liverpool Johnson dakika ya 63 yameifanya timu hiyo kufikisha pointi 70
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni