Kamanda Suleiman Kova
Watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi
wamevamia benki ya Barclays tawi la Kinondoni Jijini Dar es Salaam na
kupora kiasi kikubwa cha fedha ambazo idadi yake haijajulikana mara
moja.
Tukio hilo limetokea leo majira ya saa
nne katika tawi la benki hiyo iliyopo Kinondoni eneo la Bakwata
likihusisha watu watatu waliokuwa na pikipiki mmoja wao akiwa na
bastola.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar
es Salaam, Suleiman Kova amefika katika eneo la tukio hilo akiwa na
askari wa upelelezi ili kuchunguza tukio hilo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni