.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 13 Aprili 2014

MAKAMU WA RAIS DK. BILAL NA WAZIRI MAGUFULI WANUSURIKA KATIKA AJALI YA HELKOPTA


Makamu wa rais wa Tanzania Dk. Mohamed Gharib Bilal, Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli pamoja na RPC Suleman Kova wamenusurika katika ajali leo baada helkopta waliyokuwa wamepanda kupata hitilafu wakati ikiruka Ukonga kwenda kuangalia athari zilizosababishwa na mvua Jijini Dar es Salaam.

Wengine waliokuwemo ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Mecky Sadiki pamoja na wajumbe wa kamati ya maafa, ambapo hakuna mtu yeyote aliyejeruhiwa katika ajali hiyo na walipelekwa hospitali kuchunguzwa iwapo wamepata madhara na kuruhusiwa.


Tukio hilo limetokea leo Jijini Dar es Salaam katika uwanja wa ndege wa jeshi wa Ukonga majira ya saa tano asubuhi, ambapo viongozi hao walipokuwa wakijiandaa kupaa na helkopta hiyo na ndipo ilipopata hitilafu baada ya kuruka juu kidogo na kuanguka.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni