Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal akiwasili katika msiba wa mwanamuziki mkongwe nchini Muhidin Maalim Gurumo
Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal akisalimiana na viongozi mbalimbali alipowasili msibani hapo
Makamu wa Rais Dk. Bilal akiwapungia waombolezaji katika msiba wa mwanamuziki Muhidin Maalim Gurumo aliyefariki dunia juzi jumapili
Waombolezaji wakiwa msibani
Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal akifuatilia shughulizi zilizokuwa zinaendelea, alipofika katika msiba wa mwanamuziki mkongwe nchini Muhidin Maalim Gurumo aliyefariki siku ya jumapili katika hospitali ya Taifa Muhimbili, kabla ya kupelekwa Masaki wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani kwa mazishi yatakayofanyika leo
Mmoja wa wanafamilia akisoma wasifu wa marehemu Muhidin Maalim Gurumo " Kamanda "
Waombolezaji wakiwa msibani hapo
Kiongozi wa Msondo Ngoma Music Band, Said Mabera akisoma salaam za rambi rambi
Mwanamuziki Ally Choki akihojiwa na waandishi wa habari. Ally Choki amepata kuingia studio na kuurudia wimbo maarufu wa Kasimu akiwa Muhidin Maalim Gurumo
Sala ikiendelea msibani hapo
Msanii maarufu wa maigizo nchini, JB akiongea jambo na Mkurugenzi wa Radio One, Deogratius Rweyunga huku aliyepata kuwa meneja wa klabu ya Simba Evarist Hagilla ( katikati ) akifuatilia kwa makini
Mwili wa marehemu, Muhidin Maalim Gurumo ukiondolewa nyumbani kwake Mabibo External tayari kuelekea Masaki wilyani Kisarawe mkoani Pwani kwa maziko.














Hakuna maoni :
Chapisha Maoni