.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 18 Aprili 2014

NAHODHA WA KIVUKO KILICHOZAMA KOREA KUSINI AKAMATWA NA KUFIKISHWA MAHAKAMANI

 Nahodha wa kivuko cha Korea Kusini kilichozama jumatano amekamatwa na polisi baada ya kugundulika kuwa wakati kivuko hicho kilipoanza kuzama alikuwa ni mmoja kati ya watu waliotoka ndani ya kivuko hicho wa kwanza bila kutoa msaada kwa abiria wake. 

Nahodha huyo Leen Joon-Seok mwenye miaka 68 ( pichani juu akishuka ) ameshtakiwa kwa kuwatelekeza abiria wake na kusababisha vifo 28 na mpaka sasa bado watu 270 hawajaokolewa. 

Kivuko hicho kilikuwa na abiria 470 wengi wao wakiwa wanafunzi na kilikuwa kinaelekea kusini mwa kisiwa cha Jeju.
 Lee Joon- Seok ( katikati ) akifikishwa katika mahakama ya Mokpo kusini mwa Seoul hii leo kujibu mashitaka yanayomkabili.
                              Shughuli za uokoaji zikiendelea eneo kilipozama kivuko hicho

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni