Ndege ya shirika la ndege la Malaysia Boeing 737 iliyokuwa na abiria 159 imelazimika kutua kwa dharura muda mfupi baada ya kuruka kutoka Kuala Lumpur kuelekea Bangalore India.
Ndege hiyo namba MH 192 ililazimika kuzunguka angani kabla ya kuruhusiwa kutua tena Kuala Lumpur baada ya kutokea hitilafu katika mfumo wake wa gia muda mfupi baada ya kuruka kutoka uwanjani hapo.
Safari kutoka Kuala Lumpur kwenda Bangalore inasadikiwa kuwa dakika 90, lakini abiria iliwalazimu kukaa angani kwa zaidi ya saa nne wakizunguka anga la Kuala Lumpur wakisubiria mamlaka husika kuruhusu ndege hiyo kutua kwa dharura baada ya kuhakikisha uwanja upo salama na tayari kwa ndege hiyo kutua tena
Waziri wa Uchukuzi wa Malaysia, Hishammuddin Hussein ( mwenye kofia ) akiongea na abiria waliokuwa katika ndege hiyo baada ya abiria wote kutoka salama
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni