.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 14 Aprili 2014

NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AANZA KWA KISHINDO ZIARA YAKE YA MKOA WA KATAVI


Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (wapili kushoto) akikagua ujenzi wa bandari ya Karema wilaya ya Mpanda ambao umekwama kwa miaka mitatu sasa kutokana na mkandarasi kudaiwa kutokuwa na sifa na uwezo wa kukamilisha ujenzi huo. Kinana ametembelea ujenzi huo leo akiwa katika ziara ya siku nne mkoani Katavi kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia ya kuzitatua.
 Kinana na Nape (kulia) wakitoka kukagua ujenzi wa bandari hiyo leo
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akizungumza na waandishi baada ya kukagua ujenzi wa bandari hiyo ambapo ameahidi kuiagiza serikali kuhakikisha ujenzi huo ambao umekwama unakamilika.

 Vijana wakitumbuiza kwa matarumbeta kumlaki Kinana Ofisi ya CCM Kata ya Karema leo.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa soko la samaki la Ikola wilayani Mpanda mkoani Katavi.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa soko la samaki la Ikola wilayani Mpanda mkoani Katavi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni