Timu ya soka ya Real Madrid ya Hispania imeanza vyema harakati zake za kutaka kucheza fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya, baada ya usiku wa kuamkia leo kuitandika Bayern Munich toka Ujerumani kwa bao 1-0 katika mchezo mkali wa nusu fainali ya ligi hiyo uliochezwa katika uwanja wa Santiago Bernabeu.
Katika mchezo huo uliokuwa na ushindani mkali, alikuwa ni Karim Benzema aliyewanyanyua mashabiki wa Real Madrid waliofurika uwanjani hapo baada ya kuifungia bao hilo muhimu kunako dakika ya 19 ya kipindi cha kwanza cha mchezo, bao ambalo lilidumu hadi dakika 90 zinamalizika.
Mchezo huo uliochezeshwa na mwamuzi Howard Webb toka Uingereza, ulishuhudia kila timu ikicheza kwa kiwango cha hali ya juu na kushambuliana kwa zamu. Timu hizo zitarudiana wiki ijayo katika uwanja wa Allianz Arena huko Ujerumani
KIJANA POLE NDIO MCHEZO!! Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti akimkumbatia kocha wa Bayen Munich, Pep Guardiola baada ya mchezo huo
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni