Raia mmoja wa China, Xie Shuiping ameamua kujipatia kipato chake cha kila siku kwa kuruhusu watu wampige kadiri wawezavyo katika tumbo lake. Shuiping mwenye miaka 48 mkazi wa jimbo la Hubei, amesema kwa mwezi anaingiza kiasi cha Yuan 20,000 kutoka kwa watu mbalimbali wanaompiga ngumi au mateke katika tumbo lake.
Pamoja na kupata kipingamizi kutoka kwa mke wake na watoto wao wawili wa kike juu ya kazi yake hiyo ambayo inaweza kuhatarisha maisha yake, Shuiping amegoma kuwasikiliza na kusema kuwa kipato anachokipata kutokana na kupigwa tumboni na wapita njia mtaani, kinamsaidia sana kuendesha maisha yake na familia yake bila shida.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni