.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 6 Mei 2014

CRYSTAL PALACE YAITIBULIA MAHESABU YA UBINGWA LIVERPOOL

                    Mshambuliaji hatari wa Liverpool Suarez akimwaga chozi



Liverpool imevurunda na kujikuta ikiruhusu kufungwa mabao matatu ndani ya dakika 11 licha ya kuanza kwa kuongoza kwa mabao matatu kwa bila kwa muda mrefu katika mchezo wake na Crystal Palace ulioisha kwa sare ya mabao 3-3.



Kwa sare hiyo Liverpool inayonolewa na Brendan Rodgers imejikuta ikiharibu mahesabu ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kupokonywa ushindi jana katika dakika za mwisho na Crystal Palace katika sare hiyo.



Katika mchezo huo Liverpool ilipata bao la kwanza kupitia kwa Allen katika dakika ya 18, Sturridge dakika ya 53 na Luis Suarez dakika ya 55, ambapo mbao ya Crystal palace alifungwa na Delaney dakika ya 79, Gayle dakika ya 81 na 88.
                                                 Steven Gerrard akiwa hoi
                            Daniel Sturridge akiwa haamini kilichotokea

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni