Wasanifu wa majengo nchini Paraguay
wamesema mchwa wamevamia Ikulu ya nchi hiyo na kutishia kuathiri
jengo hilo la rais.
Msanifu majengo Gustavo Glavinich
amesema mchwa hao wameharibu maeneo yaliyojengwa kwa mbao, ikiwemo
sakafu pamoja na nguzo za mbao zinazoshikilia baadhi ya maeneo ya
jengo la Ikulu hiyo.
Glavinich amesema kuwa maeneo
mengine ya Ikulu hiyo iliyojengwa karne ya 19, si tu yana mchwa bali
pia kuna makundi ya popo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni