.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 8 Mei 2014

KESI YA PISTORIUS MTAALAM AELEZA REEVA HUENDA ALIKULA KABLA YA KUUWAWA

Siku ya 28 ya kesi ya mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius imeshuhudia mahakama ikielezwa kuwa marehemu Reeva Steenkamp huenda alikula chakula chake cha mwisho usiku alipouwawa na mpenzi wake huyo.

Shahidi Christina Lundgren, mtaalam wa mwili wa binadamu ameelezea namna tumbo la binadamu linavyoweza kuonekana likiwa halina chakula baada ya kula.

Amesema tuhuma za kuwa kulikuwa na malumbano kuwa tumbo la Steenkamp lilikuwa na chakula ama tupu wakati Pistorius alipomua zilijengwa katika uvumi mtupu.

Pistorius amekanusha kumuua kwa makusudi mpenzi wake Steenkamp Februari 14 mwaka jana.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni