.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 8 Mei 2014

MTANZANIA ANASWA NA KETE 18 ZA DAWA ZA KULEVYA KATIKA UWANJA WA JOMO KENYATTA

Mwanaume mmoja raia wa Tanzania jana amekamatwa kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta Jijini Nairobi akisafirisha dawa za kulevya aina ya cocaine zenye thamani ya shilingi milioni 1.2 za Kenya.

Mtu huyo aliyetokea Tanga na kuingia Kenya kupitia Mombasa pia alinaswa na dawa za kulevya aina ya heroine alizokuwa amezishindilia kwenye njia ya haja kubwa zikiwa na thamani ya shilingi 105,000 ya Kenya.

Mkurugenzi wa Upelelezi Joseph Ngisa amesema walimsimamisha Mtanzania huyo na kumshikilia katika uwanja wa Jomo Kenyatta baada ya kumshuku na kufanikia kutoa kete 16 za cocaine na keti mbili za heroine.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni