.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 15 Mei 2014

KLABU YA SEVILLA YATWAA UBINGWA WA LIGI YA UROPA KWA MATUTA

Klabu ya Sevilla imeifunga kwa mikwaju ya penati Benfica na kutwaa ubingwa wa Ligi ya Uropa katika mchezo uliochezwa Turin, na kuweka rekodi ya kuchukua kombe hilo mara tatu katika misimu tisa.

Matokeo hayo yameifanya Benfica, kushindwa mara saba katika michezo saba ya fainali ligi ya uropa na kukosa nafasi kulitwaa kombe hilo tangu mwaka 1962.

Mchezaji Kevin Gameiro alifunga mkwaju wa penati ya mwisho baada ya kipa wa Sevilla, Beto kupangua mikwaju ya penati ya Oscar Cardozo na Rodrigo, na kufanya matokeo kuwa mabao 4-2.
          Rais wa UEFA Michel Platini akikabidhi kikombe kwa wachezaji wa Sevilla
Wachezaji wa Sevilla wakishangilia ushindi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni