Kocha Adel Amrouche
Mamlaka inayosimamia Soka
nchini Kenya imetengua uamuzi wa kocha mkuu wa timu ya Taifa Harambee
Stars, Adel Amrouche wa kumtimua kazi msaidizi wake James Nandwa.
Mkutano uliofanyika jana
wa maafisa wa shirikisho la soka Kenya umeridhia kumrudisha kazini
Nandwa, ambaye tofauti zake na Amrouche zilikuwa zinatishia
kuzorotesha maandalizi ya Harambee Stars katika mchezo wa kuwania
kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika.
Taarifa iliyotolewa na
kikao hicho cha shirikisho la soka imeeleza kuwa ni wajibu wa
shirikisho kulinda ajira za wazawa hivyo Nandwa ataendelea kutekeleza
majukumu yake ya kusaidia kuinoa Harambee Stars.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni