Kocha wa Chelsea Jose Mourinho amesema
ni muhimu kwa timu hiyo kuongeza mshambuliaji mwenye makali ya
kucheka na nyavu, ili kufanya vyema katika msimu ujao.
Matumaini ya Chelsea kutwa Ligi Kuu ya
Uingereza yalizimwa baada ya kutoa sare ya 0-0 na timu inayokabiliwa
na tishio la kushuka daraja ya Norwich.
Pia Chelsea ilipoteza michezo yake ya
hivi karibuni dhidi ya Aston Villa, Crystal Palace na Sunderland.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni