Watu waliokuwa na visu wamewashambulia na kuwajeruhiwa vibaya abiria sita waliokuwa wakisubiri usafiri katika stesheni ya treni ya Guangzhou nchini China.
Katika tukio hilo, polisi walifanikiwa kumpiga risasi na kumkamata mmoja wa watu hao.
Taarifa zaidi juu ya tukio hilo bado haijatolewa, na tukio hilo limetokea ikiwa imepita wiki moja tu tangu kutokea kwa tukio lingine kama hilo katika kituo cha stesheni cha Urumqi, magharibi mwa mkoa wa Xinjiang.
Huu ni mfululizo wa mashambulizi, machi mwaka huu watu 29 waliuawa katika stesheni ya Kunming.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)




Hakuna maoni :
Chapisha Maoni