Madai ya Mbunge Dkt. Oburu Oginga kuwa
wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanapanga njama za kumuua
aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga yamepokelewa kwa hisia
tofauti.
Dkt. Oburu alitoa madai hayo katika
mahafali ya Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Jaramogi Oginga
Odinga, ambapo alidai wakuu hao wa nchi walikutana hivi karibuni
Jijini Nairobi kupanga njama hizo za kumua Raila.
Dkt. Oburu alinukuliwa akisema kuwa
anataarifa za uhakika kuwa viongozi hao walidai kuwa matatizo
yanayoikabili nchi ya Kenya hivi sasa yanasababishwa na Raila Odinga.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni