
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua rasmi Mkutano wa siku mbili wa Mazungumzo baina ya Viongozi wa Dini mbalimbali na Wanasiasa kuhusu ujenzi wa Demokrasia, Maendeleo na uimarishwaji wa Amani ulioshirikisha nchi za Afrika na kufanyika kwenye Hoteli ya White Sands, jijini Dar es Salaam, leo Mei 6, 2014. Picha na OMR.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa TAnzania,. Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akishiriki dua ya pamoja na baadhi ya viongozi wa dini, kutoka (kushoto) ni Katibu Mkuu wa BAKWATA, Sheikh Suleiman Loila, Askofu Dkt. Alex Malasusa na (kulia) ni Sheikh Khamis haji, wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano wa siku mbili wa Mazungumzo baina ya Viongozi wa Dini mbalimbali na Wanasiasa kuhusu ujenzi wa Demokrasia, Maendeleo na uimarishwaji wa Amani ulioshirikisha nchi za Afrika uliofanyika kwenye Hoteli ya White Sands, jijini Dar es Salaam, leo Mei 6, 2014. Picha na OMR.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni