Wataalam wa ujasusi wa
Marekani wametumwa nchini Nigeria, kusaidia kuwapata wanafunzi
wasichana zaidi ya 200, waliotekwa mwezi uliopita na kundi la Boko
Haram.
Rais Barack Obama wa
Marekani amesema timu hiyo inahusisha wanajeshi, makachero pamoja na
mawakala wa taasisi zingine za uchunguzi.
Mapema jana ilibainika
kuwa wasichana wadogo wengine wanane walitekwa Kaskazini Mashariki
mwa Nigeria na wapiganaji.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni