.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 12 Mei 2014

MASHABIKI WA AFC LEOPARDS WALETAFUJO NA KUSABABISHA MECHI KUVUNJIKA

Mashabiki wakorofi wa timu ya AFC Leopards wamevamia uwanja na kupelekea kuvunjika kwa mchezo wao wa Ligi Kuu ya Kenya dhidi ya Thika United ulichezwa jana katika uwanja wa Taifa wa Nyayo.

Tukio hilo limetokea mnamo dakika ya 85, wakati Thika United ikiwa inaongoza kwa bao moja kwa bila dhidi ya AFC Leopards, lililopachikiwa kimiani na Dennis Odhiambo mnamo dakika ya 10.

Wakati mchezo huo ukielekea kuisha baadhi ya mashabiki wa AFC Leopards walianza kurusha chupa za maji uwanjani kabla ya kuvamia uwanjani na kumlazimisha refa Nasur Doka kumaliza mechi hiyo baada ya kushauriana na wasaidizi wake.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni