Nishikori na Nadal wakipozi kwa picha
Mchezaji tenesi Rafael Nadal ameshinda
taji lake la kwanza katika michuano ya tenesi ya Ulaya iliyochezwa
kwenye uwanja wa udongo, wakati maumivu ya mgongo yakimlazimisha
Mjapan Kei Nishikori kushindwa kumalizi mchezo huo wa fainali huko
Madrid.
Mchezaji huyo wa dunia anayeshika
nafasi ya kwanza katika mchezo wa tenisi aliongoza wa seti 2-6 6-4 3-0 wakati Nishikori
aliyeongoza seti ya kwanza akishindwa kuendelea na kujitoa.
Mrusi Maria Sharapova amefanikiwa
kuondoa hofu na kumshinda Simona Halep wa Romania katika mchezo wa
finali za Michuano ya Wazi ya Tenesi ya Madrid na kutwa ubingwa.
Mchezaji huyo aliyewahi kushika nafasi
ya namba moja katika mchezo huo alipambana na kushinda kwa seti 1-6
6-2 6-3 na kuongeza rekodi yake ya kutoshindwa katika michuano ya
uwanja wa udongo katika michezo 11.
Maria Sharapova akishangilia ushindi wake


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni